Home Top Ad

Responsive Ads Here

wanasayansi kugundua bara lingine

Unayafahamu mabara yote saba? Jiandae sasa, kuna bara jingine ambalo huenda likaongezwa.
Bara hilo limependekezewa jina Zealandia.
Ni sehemu kubwa ya ardhi ambayo inakaribia kabisa kufunikwa na maji ya bahari kusini magharibi kwa bahari ya Pasifiki.
Kinachoonekana kwa sasa ni sehemu ya juu pekee ya milima kwenye bara hilo, ambayo hujitokeza juu ya maji ya bahari kwama visiwa ambavyo huitwa New Zealand.
Wanasayansi wanasema sehemu hiyo ya ardhi inatosha kuitwa bara na sasa wamefufua juhudi za kutaka litambuliwe rasmi kama bara.
Kwenye makala waliyochapisha katika jarida la masuala ya jiolojia Marekani la Geological Society of America, watafiki hao wanasema ukubwa wa Zealandia ni kilomita milioni tano mraba. Hiyo ni kama theluthi mbili ya bara lililo karibu la Australia.
Takriban 94% ya sehemu hiyo ya ardhi imo chini ya maji ya bahari na ni visiwa vitatu pekee vilivyochomza juu ya maji ambavyo hufahamika kama Visiwa vya Kaskazini na Visiwa vya Kusini nchini New Zealand na visiwa vya New Caledonia.
Huenda ukadhani ardhi kuwa juu ya bahari ni kigezo muhimu cha sehemu ya ardhi kuitwa bara, lakini watafiti hao wanaangazia sifa tofauti zikiwemo.
  • Mwinamo wa maeneo yanayopakana na bara hilo
  • Eneo kuwa la kipekee kijiolojia
  • Hali kwamba eneo husika linaweza kutenganishwa na maeneo mengine
  • Kuwa na gamba lake kuwa na pana kuliko gamba la kawaida baharini

Mtafiti mkuu, mwanajiolojia kutoka New Zealand Nick Mortimer, amesema watafiti wamekuwa wakitafuta data ya kutetea Zealandia kutambuliwa kuwa bara kwa miongo miwili.
Iwapo mpango wao utafanikiwa, wachapishaji wa vitabu wanafaa kuwa na wasiwasi kwamba watahitaji kufanya marekebisho?
Kumbuka miaka michache iliyopita Pluto iliondolewa kwenye orodha ya sayari kwenye mfumo wa jua.
wanasayansi kugundua bara lingine wanasayansi kugundua bara lingine Reviewed by Unknown on 11:34:00 Rating: 5

No comments

Recent