Home Top Ad

Responsive Ads Here

Ben Pol afunguka juu ya Tunda

Msanii Ben Pol amefunguka na kuweka sawa juu ya tetesi ambazo zipo mtaani kuwa anatoka na video queen Tunda ambaye sasa inasemakana anatoka na rapa Young Dar es Salaam.
Ben Pol alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) alisema yeye alikuwa na urafiki wa mbali sana na Tunda na kusema hizo tetesi hazina ukweli kwani Tunda alikuwa rafiki wa karibu wa mdogo wake na si yeye.
"Siyo kweli sijawahi kuwa na mahusiano na Tunda nachojua mimi Tunda alikuwa karibu na mdogo wangu mimi yaani rafiki yangu wa karibu anaitwa Tonny Dagi, ndiyo alikuwa naye karibu sana, sijawahi kujua kama Tunda anajihusisha na mambo ya madawa ya kulevya sababu sijawahi kuwa karibu naye kivile, kusema nimekaa naye hata masaa sita au manne sijawahi kukaa naye karibu" alisema Ben Pol 
Mbali na hilo Ben Pol alizungumzia suala la video Queen huyo kuhusishwa na madawa ya kulevya, anadai kama ni kweli anajihusisha na mambo hayo si jambo zuri sababu tayari yule amekuwa kioo cha jamii kuna mabinti wengi wanamuangalia na wengine wanatamani kuwa kama yeye hivyo si jambo jema yeye kuwa huko.
"Kama ametajwa kweli na anafanya hivyo vitu, kiukweli siyo kitu kizuri haileti picha nzuri yeye ameshakuwa na impact kubwa, mabinti wengi wanamuangalia, wengine wapo mashuleni huko wanatamani kuwa kama yeye, kuwa ma models, wanajulikana kwa hiyo haiwezi kuleta picha nzuri kama ni kweli inabidi aache" alisema Ben Pol  
Ben Pol afunguka juu ya Tunda Ben Pol afunguka juu ya Tunda Reviewed by Unknown on 01:56:00 Rating: 5

No comments

Recent